Kilichogunduliwa 14: Msaada wa Marekani unaolenga sekta ya utawala husaidia Kenya kubuni vishawishi vinavyofaa ili maafisa wake waliochaguliwa waboreshe jinsi wanavyotoa huduma na kushughulikia mahitaji ya wananchi.

Ruwaza ya Kenya ya 2030 inatoa wito kwa nchi hiyo “kusonga mbele kwa umoja” na kushinda historia ya utengano wa kisiasa na mapendeleo ya kikabila na kidini wakati ambapo huduma zinatolewa (Masakhalia, 2011; Wanjobi, 2014). Chini ya uongozi wa Rais Uhuru Kenyatta, Kenya imejitolea kuhakikisha kwamba uwakilishi unahusisha sauti za watu mbalimbali (k.m., misimamo mbalimbali ya kisiasa, makabila mbalimbali) wakati wa kufanya maamuzi, kuimarisha asasi za kiraia, kuimarisha uwazi, na kufanikisha majadiliano mazuri ya kisiasa, miongoni mwa mambo mengine.

Marekani na Kenya zinaunganishwa na nia moja ya kuchangia katika utawala bora na kuimarisha taasisi za kidemokrasia ambazo zinahusisha Wakenya wote. Katika kipindi cha miongo miwili iliyopita, serikali ya Marekani imetekeleza mipango 37 ya msaada wa kiufundi na kuelekeza zaidi ya Dola milioni 257 kwenye shughuli zinazounga mkono na kuimarisha mifumo ya utawala bora nchini Kenya (tazama Mchoro wa 15). Kati ya 2014 na 2018, Marekani ilielekeza takriban Dola milioni 19.6 kila mwaka katika shughuli za demokrasia, haki za kibinadamu, na utawala.

Mchoro wa 15. Msaada wa demokrasia, utawala bora na haki za kibinadamu, uliotolewa kwa Kenya na serikali ya Marekani, 2001-2018

0 5 10 15 20 25 $ milioni 30 18 15 10 05 2001

Maelezo: Grafu hii inaonyesha pesa zilizotolewa kwa Kenya kupitia msaada rasmi wa maendeleowa Marekani zilizoelekeza katikademokrasia, utawala bora na haki za kibinadamu kati ya mwaka wa 2001 na 2018 kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya Dola ya 2019.

Asili: USAID Foreign Aid Explorer Data.

Shughuli za kukuza utawala bora, kwa kawaida, huchukua miaka mingi kuzaa matunda, lakini Kenya tayari imeshapiga hatua muhimu katika suala hilo. Kenya imetoa nafasi kwa idadi inayoongezeka ya sauti mbalimbali za kisiasa Katika miaka ya nyuma, nchi hiyo ilikuwa nchi yenye chama kimoja (1982-1991), lakini Wakenya waliunda vyama 17 vipya vya kisiasa kati ya mwaka wa 2000 na 2009, na zaidi ya vyama 14 vimesajiliwa kuanzia 2010 hadi sasa. Kwa sasa, wananchi wamekuwa na fursa nzuri zaidi ya kuhakikisha sauti zao zinasikika katika debe la kura, kwa sababu kumekuwa na ongezeko thabiti katika viwango vya uwezo wa kuchagua kiongozi unayemtaka katika chaguzi zenye haki na uhuru katika mwongo mmoja uliopita. Hiyo ni kwa mujibu wa Kielezo cha Bertelsmann cha Mabadiliko ya Kenya (Bertelsmann Transformation Index for Kenya (BTI, 2018).

Chaguzi zenye ushindani na wawakilishi mbalimbali wa kisiasa hutoa vishawishi bora kwa viongozi waliochaguliwa kuboresha ufikiaji wa huduma na kushughulikia mahitaji ya wapigaji kura (Sen, A. 1999; Mehrotra, S. 2008). Kwa hivyo, tunatarajia kuona wananchi wengi zaidi wakiweza kufikia huduma na wakiridhika na serikali sambamba na sauti mbalimbali za kisiasa zinazozidi kuongezeka nchini Kenya na unedeshaji wa chaguzi huru na zenye haki.

Katika hali hiyo, ni jambo la kutia moyo sana kuona kwamba nyumba nyingi za Kenya zinaripoti kwamba zinaweza kupata maji safi (ongezeko la asilimia 15) na umeme (ongezeko la asilimia 40) kati ya mwaka wa 2000 na 2017, kulingana na Benki ya Dunia (WDI, n.d.). Wakenya pia wamezidi kuwa na matumaini kwamba serikali yao inaweza kutoa huduma hizi muhimu na wamezidi kuamini viongozi wao wa serikalini. Habari za hivi majuzi za utafiti wa Afrobarometer zinasema kwamba karibu asilimia 70 ya wananchi wa Kenya wanaamini kwamba serikali inashughulikia vizuri hitaji la umma la umeme katika mwaka wa 2018, asilimia hiyo ikiwa imeongezeka kutoka asilimia 45 katika mwaka wa 2008. Pia, tafiti za kubaini maoni ya raia zinazotekelezwa kila mwaka na Gallup World Poll zinazonyesha kwamba idadi ya wananchi ambao wana imani na serikali ya Kenya imeongezeka, kutoka asilimia 25 katika mwaka wa 2009 hadi karibu asilimia 70 katika mwaka wa 2019.

Kenya bado ina kazi nyingi sana ya kufanya ili kutimiza malengo yake ya Ruwaza ya 2030. Hata hivyo, nchi hiyo imeshapiga hatua kubwa kwa kuunda nafasi za kisiasa kupitia kuwa na vyama mbalimbali vya kisiasa na kuendesha chaguzi huru zenye haki. Maendeleo haya ya kisiasa pia yanaambatana na kuimarika kwa ufikiaji wa huduma muhimu na wananchi kuzidikuwa na imani kwamba serikali itashughulikia mahitaji yao. Kuna vitu vingi ambavyo vinasaidia Kenya kutimiza malengo yake ya utawala bora, lakini tunaweza kusema kwamba nchi ya Marekani imekuwa mshirika muhimu sana Kenya inapojitahidi kutimiza malengo hayo kwa kutoa msaada muhimu wa kifedha na kiufundi.

Kilichogunduliwa 15: Msaada wa Marekani unaolenga sekta ya kilimo huimarisha uzalishaji katika maeneo ya mashambani ya Kenya ili kuongeza mapato na kupunguza ukosefu wa usawa.

Kadiri Kenya inavyoazimia kuwa taifa ambalo linaendelea kwa kasi lenye pato la kati ifikapo 2030, kuimarisha sekta yake ya kilimo ili iwe ya kisasa kwa lengo la kuongeza mavuno ya mazao kutakuwa ni hatua muhimu si tu katika kuhakikisha kwamba kuna chakula cha kutosha nchini, bali pia katika kuimarisha maisha ya raia wanaoishi mashambani. Marekani imekuwa mshirika muhimu katika kutoa msaada wa kifedha na kiufundi kwa sekta ya kilimo ya Kenya, kupitia mipango yake ya kutoa msaada kati ya nchi mbili na kutoa msaada wa kimataifa (tazama Mchoro wa 16), pamoja na kupitia mikopo midogo, ruzuku, na usaidizi wa kiufundi kutoka kwa mashirika na watu binafsi kutoka Marekani.

Mchoro wa 16. Msaada wa Marekani kwa kilimo na mazao ya sekta ya kilimo ya Kenya, 2008-2018

5 10 15 20 $ bilioni 25 20 40 60 80 $ milioni 100 2018 2015 2010 2008 Uzalishaji wa kilimo Msaada wa kilimo kati ya nchi mbili

Maelezo: Grafu hii inaonyesha jumla ya mazao ya sekta ya kilimo ya Kenya kati ya 2008 na 2018 kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya Dola ya 2019.

Asili: World Development Indicators, the World Bank.

Karibu robo tatu ya watu wa Kenya wanategemea kilimo ili wapate kipato chao chote au sehemu ya kipato chao (USAID Kenya, n.d.). Kilimo pia kinaletea uchumi wa Kenya mapato makubwa sana: kilichangia asilimia 34 ya Pato la Taifa - GDP ya nchi hiyo katika mwaka wa 2018, asilimia hiyo ikiwa imeongezeka kutokea asilimia 22 katika mwaka wa 2008. [29] Hivyo, hii inaonyesha kwamba uchumi wa Kenya ni thabiti, kwani, Pato la Taifa (GDP) la Kenya lilipata kukua kwa asillimia 5.15 kwa wastani katika kipindi hicho. [30]

Kwa sasa, mapato ya wastani ya kila raia yameongezeka kutoka takriban Dola 1,050 katika mwaka wa 2008 hadi takriban Dola 1,400 katika mwaka wa 2018 [31] na ukosefu wa usawa kimapato umepungua tangu miaka ya 1990 (Jedwali la 4). Ingawa vitu vingi vinaweza kuchangia kuongezeka kwa mapato na kupungua kwa ukosefu wa usawa, kwa vile idadi kubwa ya Wakenya inategemea sekta ya kilimo kwa riziki yao, hiyo inamaanisha kwamba angalau baadhi ya maongezeko hayo yametokana na kuongezeka kwa mazao ya kilimo na mapato mengine yanayohusiana na kilimo.

Msaada wa Marekani umesaidia Kenya kuimarisha mazao yake ya kilimo kwa njia kadhaa muhimu. Mojawapo ya vitu ambavyo Marekani imesisitiza katika kutoa msaada wake ni kwamba mbinu bora za kilimo zitumiwe, ili wakulima waweze kuzalisha kiwango kikubwa cha mavuno na kupunguza vurugu vinavyotokana na hali mbovu za anga zisizotabirika. Hiyo huletea Kenya manufaa pande mbili kwani wanakuwa wameimarisha uhakika wa chakula kupitia kuwepo kwa vyakula muhimu vya kutosha—kitu ambacho kimepatiwa kipaumbele kufuatia ukame wa Afrika Mashariki wa 2011-2012— na pia wanakuwa wamesaidia wakulima kupunguza hatari kutokana na kupunguza hasara za kimapato. Kitu cha pili ambacho Marekani imesisitiza katika kutoa msaada wake ni kuwasaidia wakulima wadogo waweze kufikia masoko ya kimataifa ya bidhaa nje. Mikataba ya biashara kama vile AGOA imechangia mazingira mazuri kwa wakulima wa Kenya ya kuongeza mapato yao.

Jedwali la 4: Kizigeu wiano kati ya vipimo viwili cha GINI cha Kenya cha kupima ukosefu wa usawa wa kimapato

Mwaka GINI
1992 57.5
1994 43.1
1997 45.0
2005 46.5
2015 40.8

Maelezo: Kizigeu wiano kati ya vipimo viwili cha Gini ni kigezo kinachotumiwa kupima kiwango cha ukosefu wa usawa wakati wa kugawa mapato ya familia katika nchi fulani. Jedwali hili linaripoti Kizigeu wiano kati ya vipimo viwili cha Gini cha Kenya kuanzia 1992 hadi 2015. Vizigeu wiano kati ya vipimo viwili vya juu vinakuwepo ikiwa kuna viwango vya juu vya ukosefu wa usawa wa kimapato, ilihali vizigeu wiano kati ya vipimo viwili vya chini vinaashiria viwango vya chini vya ukosefu wa usawa.

Asili: World Development Indicators, The World Bank.