Sura ya Nne Je, ni faida gani halisia na zinazofikiriwa ambazo Kenya inapata kutokana na ushirikiano wake na Marekani?

Kufikia hapa, tumeangazia michango ya Marekani katikamaendeleo na ustawi wa Kenya kwa njia mahususi kabisa —dola zilizohamasishwa kila mwaka kwa wastani kupitia baadhi ya vyanzo vya umma, vya kibinafsi na vya watu binafsi. Hata hivyo, ushirikiano kati ya Marekani na Kenya unahusu mengi zaidi mbali na fedha. Mwishowe, nchi zote mbili zina nia moja ya kuona kwamba Kenya inaendelea kwa njia halisi na kutimiza malengo yake ya kiuchumi, kijamii na kiutawala sambamba na mpango wake wa Ruwaza ya 2030.

Katika sura hii, tunaangazia maendeleo ya Kenya katika nyanja tatu muhimu ambapo Marekani imehusika—afya, demokrasia na utawala, na kilimo—ili kugundua jinsi ambavyo kushirikiana na Marekani kunaweza kuchangia katika maendeleo ambayo Wakenya wanaona katika maisha yao ya kila siku. Pia tulitafiti viongozi wa Kenya wanaofanya kazi katika sekta 14 na makundi 5 ya wadau ili kukadiria jinsi ambavyo walichukulia michango ya Marekani ya kuisaidia Kenya kutimiza malengo yake. Kura yetu ya Maoni ya Haraka ya 2020 ya Kenya iliwaomba viongozi wa sekta ya umma, sekta ya kibinafsi na viongozi wa asasi za kiraia watoe maoni yao kuhusu kiwango cha ushiriki wa Marekani wanachoona katika sekta zao, umuhimu wa michango ya Marekani katika maendeleo ya Kenya, na mfano wa maendeleo wanayopendelea kwa ajili ya nchi yao.

Sehemu ya 4.1 Je, ni jinsi gani ushirikiano kati ya Marekani na Kenya unafaidi raia wa Kenya katika maisha yao ya kila siku?

Ili kujibu swali hili, tunaangazia mifano mitatu tofauti kwenye sekta ambazo Marekani imezitolea kiwango kikubwa cha usaidizi wake wa kifedha na kiufundi katika kipindi cha miongo miwili iliyopita:

  • Kwanza, tunaangalia utendakazi wa Kenya katika suala la kuzuia na kutibu HIV/UKIMWI ili kutimiza malengo yake ya kijamii na kiafya. Sekta ya Kenya ya afya kwa ujumla, hasa jitihada zake za kupambana na HIV/UKIMWI, kihistoria, zimevutia usaidizi mkubwa kabisa kutoka kwa jamii nzima ya Marekani (kutoka kwa serikali na vyanzo visivyo vya serikali).
  • Pili, tunaangazia utendakazi wa Kenya katika kuimarisha mifumo yake ya kidemokrasia ili kutimiza malengo yake ya kisiasa na kiutawala. Marekani imehamasisha msaada mkubwa wa kifedha na kiufundi katika miaka ambayo imepita ili kuunga mkono uchaguzi wenye ushindani na uwakilishi wa kisiasa unaohusisha watendaji mbalimbali ili kuleta vichocheo vizuri vitakavyosababishavya huduma za umma zitolewe ipasavyo na kwa usawa kwa watu wote wa Kenya.
  • Tatu, tunaangazia utendakazi wa Kenya katika sekta ya kilimo, ambapo washiriki mbalimbali wa Marekani, ikiwemo serikali, wanachangia na kuhusika kupitia usaidizi wa kiufundi, mikopo midogo midogo, na ruzuku.

Kilichogunduliwa 13: Msaada kutoka Marekani unaolenga sekta ya afya husaidia sio tu kuokoa maisha ya watu pekee, bali pia huchangia katika uzalishaji wa uchumi wa Kenya, kadiri watu wanavyofanya kazi kwa muda mrefu zaidi.

Wafanyakazi wenye afya wanaofanya kazi vizuri wanahitajika ili kutimiza ndoto ya Kenya ya muda mrefu ya kuwa taifa lenye ushindani wa kimataifa na ustawi ifikapo 2030.Katika hali hiyo, janga la HIV/UKIMWI ni “mojawapo ya matishio makubwa zaidi kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii” (Baraza la Kitaifa la Kudhibiti Ukimwi - National Aids Control Council, 2020). Kwa mfano, Kenya ilishuhudia ongezeko mkubwa wa maambukizo mapya ya HIV mwishoni mwa miaka ya 1990, na ikawa mojawapo ya nchi kadhaa za Afrika zenye idadi kubwa ya wagonjwa wa HIV.

Kufuatia idadi kubwa ya vifo vilivyotokana na UKIMWI katika mwaka wa 2004, Kenya imejiimarisha katika kuzuia vifo vinavyotokana na ugonjwa huo (tazama Mchoro wa 13), na imepunguza idadi ya maambukizo mapya ya HIV kwa asilimia 55 tangu 2010 (UNAIDS, 2020). Uwezo naozidi kuimarika wa Kenya katika kufanikisha mipango ya uzuiaji na matibabu—kama vile kupeana matibabu ya kudhibiti virusi (ART) kwa watu wengi zaidi walioathiriwa (tazama Mchoro wa 13), na kuwawezesha watu kupata huduma ya afya kwa bei nafuu—ni vipengele muhimu katika mafanikio hayo.

Mchoro wa 13. Vifo vinavyotokana na UKIMWI nchini Kenya (1995-2016) na asilimia ya watu wanaoishi na HIV wanaopokea ART (2010-2016)
50,000 100,000 150,000 200,000 250,000 20 40 60 80 100% Asilimia ya watu wanaoishi na HIV wanaopokea ART Vifo vinavyotokana na UKIMWI 2016 2010 2005 2000 1995

Maelezo: Mstari mwekundu unaonyesha idadi inayokadiriwa ya vifo vinavyotokana na UKIMWI nchini Kenya kati ya 1995 na 2016, na ishara husika kwamba idadi hiyo itaendelea kupungua. Mstari wa kijani unaonyesha asilimia inayokadiriwa ya watu wanaoishi na HIV wanaopokea ART nchini Kenya kati ya 2010 na 2016, na ishara husika kwamba idadi hiyo itaendelea kuongezeka.

Asili: UNAIDS 2019 Estimates.

Tunakadiria kwamba jitihada za kupambana na HIV/UKIMWI nchini Kenya zimesaidia kuokoa zaidi ya maisha milioni moja kufikia leo.[28] Zaidi ya hiyo, kwa vile wastani wa umri wa kuishi wa Kenya umeongezeka katika kipindi cha miongo miwili iliyopita—kutoka miaka 51 katika mwaka wa 2000 hadi miaka 66 katika mwaka wa 2018 (tazama Mchoro wa 14)—hiyo inamaanisha pia kwamba kila Mkenya amepata ongezeko la wastani wa miaka 15 yauzalishaji wa kiuchumi.

Mchoro wa 14. Muda unaotarajiwa wa maisha kuanzia wakati wa kuzaliwa nchini Kenya, 1995-2017
50 52 54 56 58 60 62 64 66 68 70 16 10 05 00 1995

Maelezo: Grafu hii inaonyesha wastani wa umri wa kuishi wa Wakenya kuanzia wakati wa kuzaliwa kutoka 1995 hadi 2017.

Asili: World Development Indicators, The World Bank.

Ushirikiano kati ya Kenya na Marekani umesaidia sana katika kuhamasisha rasilimali na utaalamu wa kuwasaidia wafanyakazi wa afya walioko kwenye mstari wa mbele kufanikisha jitihada zao za kupambana na janga la HIV/UKIMWI. Tangu 2000, serikali ya Marekani imeelekeza msaada mkubwa wa kiufundi na fedha katika sekta ya afya ya Kenya (tazama Mchoro wa 3). Kiwango kikubwa cha mchango huu kimetumiwa kupambana na HIV/UKIMWI nchini Kenya na kuhakikisha kwamba ART zinapatikana. Kwa kweli, serikali ya Marekani ndio imetoa msaada mkubwa zaidi kati ya watoaji msaada wote wa kimataifa kwa ajili ya matibabu na udhibiti wa HIV/UKIMWI nchini Kenya.

Ni muhimu kutaja kwamba kwa kufanya tathmini hii hatumaanishi kwamba tumetathmini ufanisi wa shughuli mahususi za maendeleo, ambalo ni jambo lisiloshughulikiwa kwenye utafiti huu, na kwamba sababu nyinginezo pia huenda zimechangia katika kupungua kwa vifo vinavyotokana na HIV/UKIMWI nchini Kenya. Licha ya hiyo, kwa vile ongezeko la idadi ya watu wanaopata matibabu ya ART nchini Kenya linalingana na kuongezeka kwa msaada wa Marekani katika suala hili na pia kupungua kwa vifo, tunaweza kusema kwamba ushirikiano kati ya Kenya na Marekani unawaletea watu wa Kenya faida kupitia kuboreka kwa hali ya maisha na kuongezeka kwa maendeleo ya kiuchumi.