Sehemu ya 3.3 Uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja ambao unakuza ustawi nchini Kenya

Kampuni za Marekani zinazidi kuichukulia Kenya kama pahali ambapo wanaweza kuwekeza: zinajenga majengo mapya, zinaimarisha shughuli zinazoendelea kwa sasa na zinachangia katika kutoa nafasi za kazi za utengenezaji wa bidhaa sambamba na malengo ya Kenya ya kuendeleza uchumi wake ambao wafanyakazi wake wengi ni raia wa Kenya.

Kilichogunduliwa 10: Kampuni za Marekani zimechangia takriban Dola milioni 294.2 kila mwaka katika uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja (FDI), na hivyo kuunda nafasi 1,009 mpya za kazi humo nchini kila mwaka tangu 2015 ili kuendeleza uchumi wa Kenya.

Tangu 2010, kampuni 85 za Marekani zimewekeza takriban jumla ya Dola bilioni 2.93 nchini Kenya kupitia uwekezaji mashambani na ununuzi wa mali halisi (badala ya kuungana na kununua au kukodi majengo/vituo vilivyopo). Uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja huwa tofauti kila mwaka, lakini kampuni za Kimarekani zimezalisha takriban Dola milioni 294.2 kila mwaka kama mtaji wa uwekezaji na nafasi 1,009 mpya za kazi kila mwaka tukikadiria kuanzia mwaka wa 2015 na kuendelea ili kufaidi uchumi wa Kenya (Financial Times, n.d.). Marekani ndio nambari moja kati ya nchi zote katika kuchangia nafasi za kazi ambazo Wakenya wanafanya. Jedwali la 3 linaonyesha kampuni kumi bora zaidi za Kimarekani katika uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja kwa msingi wa wa thamani ya dola zilizowekezwa kati ya 2010 na 2019.

Jedwali la 3. Makampuni 10 bora zaidi ya Marekani yanayowekeza nchini Kenya, 2010-2019

Nafasi Kampuni Sekta Jumla ya uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja
(kwa msingi wa mamilioni ya Dola)
Nafasi za kazi zilizochangiwa kwa kukadiria
1 Cummins Nishati inayoweza kutumiwa upya Dola 460 251
2 Dupre Investments Usafirishaji na mabohari Dola 398 216
3 General Electric (GE) Nishati inayoweza kutumiwa upya, vifaa vya matibabu, usafirishaji na mabohari Dola 359 80
4 Coca-Cola Vyakula na vinywaji Dola 243 2,616
5 IBM Huduma za programu na Teknolojia ya habari Dola 127 359
6 Ormat Technologies Nishati inayoweza kutumiwa upya Dola 104 60
7 Alternet Systems OEM ya Usafirishaji usiotegemea injini Dola 73 1,361
8 Mars Vyakula na vinywaji Dola 65 847
9 MasterCard Huduma za kifedha, huduma za program tumizi na teknolojia ya habari Dola 62 91
10 Microsoft Huduma za programu na teknolojia ya habari USD 55 83

Maelezo: Jedwali hili linafafanua dola za uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja na kazi za ndani ya nchi zilizochangiwa na kampuni10 kubwa zaidiza Marekani zinazoendesha shughuli zao nchini Kenya kulingana na kiasi cha uwekezaji wao. Dola za uwekezaji wa moja kwa moja ni wa mamilioni na ni kwa msingi wa thamani isiyobadilika yaDola ya 2019.

Asili: Financial Times fDi Markets database.

Nishati inayoweza kutumika upya, usafirishaji na shughuli za mabohari, na viwanda vya chakula na vinywaji vilivutia kiwango kikubwa kabisa cha mtaji wa uwekezaji wa Kimarekani, jumla yake ikiwa ni Dola bilioni 1.8 zilizowekezwa tangu 2010 (tazama Mchoro wa 10). Nafasi za kazi zilichangiwa zaidi na shughuli za utengenezaji kwenye viwanda vya vyakula na vinywaji na usafirishaji, ikifuatwa na huduma za program tumizi na teknolojia ya habari. Huku uwekezaji ukizidi kuongezeka kutoka kwa kampuni bora zaidi za teknolojia za Marekani kama vile Oracle na Microsoft, na uwekezaji wa hivi majuzi kabisa kutoka kwa Amazon na Facebook, kampuni za Kimarekani zimewekeza katika teknolojia za baadaye pamoja na shughuli za kawaida za utengenezaji.

Mchoro wa 10. Jumla ya uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja kutoka Marekani kwenda Kenya na nafasi za kazi kisekta, 2010-2019

sekta nyingine 17 Huduma za kifedha Huduma za biashara Vyakula & vinywaji Usafirishaji & mabohari Nishati inayoweza kutumiwa upya $ milioni 896.5 455.9 425.7 274.3 170.3 708.2
sekta nyingine 17 Huduma za kifedha Huduma za biashara Huduma za programu na teknolojia ya habari OEM ya Usafirishaji usiotegemea injini Vyakula & vinywaji kazi 4529 1361 939 680 475 2104

Maelezo: Grafu hizi mbili zinaonyesha kisekta jumla ya dola za uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja na jumla ya nafasi za kazi zilizozalishwa katika uchumi wa Kenya na kampuni za Marekani zinazowekeza nchini Kenya. Viwango vya Dola ni kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya Dola ya 2019.

Asili: Financial Times fDi Markets database

Sehemu ya 3.4 Dola za watalii wanaotokea Marekani na zinazotumwa humo nchini zinazofaidi uchumi wa Kenya Biashara ya utalii kutoka Marekani na malipo kupitia sarafu ya Dola ambayo yanafaidi uchumiwa Kenya

Utalii ni biashara inayofanya vizuri sana nchini Kenya, na Marekani ni mojawapo ya nchi ambazo wananchi wake wanatembelea Kenya sana, jambo ambalo huchangia mapato mazuri yanayoendeleza uchumi wa Kenya. Marekani, kwa upande mwingine, pamekuwa pahali ambapo Wakenya wanafurahia kuishi na kufanya kazi. Wakenya hawa huhusiana kwa ukaribu sana na nchi yao asilia, kama vile huwa wanatuma pesa kwa familia zao na jamii zao. Kama Benki Kuu ya Kenya (2017) Inavyosema, “pesa hizi zilizotumwa nchini kwa sasa zinatambuliwa kwamba zinachangia pakubwa katika ukuaji na maendeleo ya nchi,” kwa vile zinaweza kuimarisha maisha na kuwezesha uwekezaji mpya. Katika sehemu hii, tunaangazia, jinsi ambavyo mapato kutokana na watalii wa Marekani na pesa zilizotumwa nchini Kenya na Wakenya wanaoishi Marekani zinachangia katika maendeleo na ustawi wa Kenya sambamba na Ruwaza ya 2030.

Kilichogunduliwa 11: Watalii wanaotembelea Kenya kutoka Marekani huchangia takriban Dola milioni 190.7 kila mwaka katika uchumi wa Kenya kupitia utalii wenyewe na ada zinazohusiana na kupewa viza.

Kati ya 2013-2017, asilimia 15.4 ya jumla ya biashara nje ya kila mwaka ya Kenya kwa wastani imekuwa utalii wa kimataifa (WDI). Watalii wa Marekani huwa ni takriban asilimia 10 ya watalii milioni 1.1 ambao hutembelea Kenya kutoka kote ulimwenguni kila mwaka, jambo ambalo linachangia takriban Dola milioni 190.7 kutoka Marekani kila mwaka kwenye uchumi wa Kenya (angalia Mchoro wa 11).

Mchoro wa 11. Watalii wa marekani na mapato waliyochangia Kenya, 2009-2017

50 100 150 200 $ milioni 250 30,000 60,000 90,000 120,000 150,000 Thamani ya utalii kutoka Marekani Idadi ya watalii kutoka Marekani 2017 2016 2015 2014 2013 2012 2011 2010 2009

Maelezo: Grafu hii inaonyesha jumla ya idadi ya watalii wa Marekani waliozuru Kenya kila mwaka kati ya 2009 na 2017 (mstari wa samawati), pamoja na mapato ya kukadiriwa yaliyoletwa na watalii hawa wa Marekani katika kipindi hicho hicho, Viwango vya Dola ni kwa msingi wa thamani isyobadilika ya Dola ya 2019 (nguzo za kijani).

Asili: Ministry of Tourism & Wildlife, Govt. of Kenya.

Kwa vile Kenya ni nchi nambari tatu kusini mwa sahara ambayo uchumi wake unategemea utalii, asilimia 9.3 ya waajiriwa wameajiriwa kwenye sekta ya utalii (World Travel and Tourism Council, 2019). Hoteli, safari za mbugani, bidhaa zilivyotengezwa kwa mikono, na viwanda vingine hutoa fursa za kupata riziki kwa Wakenya wenye kipato kidogo na kipato cha kati ili kuwasaidia kuhakikishia familia zao maisha bora katika siku sijazo.

Mbali na watalii wa Marekani kutumia pesa zao moja kwa moja kwenye uchumi wa Kenya, watalii hawa pia huchangia katika mapato ya serikali ya Kenya kupitia ada za viza na za usimamizi. Mchango huo ni takriban Dola milioni 5 kila mwaka, kupitia ada za viza na za usimamizi zinazotozwa watalii Wamarekani.

Kilichogunduliwa 12: Wakenya walioko ng’ambo wanaoishi na kufanya kazi nchini Marekani walituma takriban Dola milioni 517.6 kila mwaka kwa familia na jamii zao.

Katika Sura ya 2, tulijadili idadi ya wanafunzi, wasomi na wafanyakazi wa Kenya wanaoishi nchini Marekani, iwe wanaishi kwa muda mfupi au kwa kipindi cha kudumu. Wengi wa Wakenya hawa wanaoishi ng’ambo huendelea kudumisha uhusiano wa karibu na familia na jamii zao nchini Kenya, kwa kutuma pesa zinazotumwa kutoka ugenini: mfanyakazi wa kigeni anatuma pesa kwa mtu binafsi aliye katika nchi yake ya asili. Pesa hizi zinazotumwa nyumbani ni msaadamuhimu sana wa kifedha kwa wanafamilia ili kuwapunguzia matatizo ya kifedha au kuwa nyongeza ya mapato yao. Fedha hizo pia zinaweza kuwa mtaji wa ujasiriamali wa mtu binafsi au mtaji wa kuwekeza katika biashara au mali zisizohamishika nchini Kenya.

Marekani ndio nchi nambari mbili kati ya nchi ambazo zinatuma pesa zaidi nyingi nchini Kenya. Watu binafsi, familia na biashara za Kenya zilipokea kiwango wastani cha Dola milioni 517.6 kila mwaka kutoka kwa watumaji pesa nchini Marekani kati ya mwaka wa 2013 na 2017 (tazama Mchoro wa 12). Pesa hizi zinazotumwa nchini Kenya kutoka Marekani zimeongezeka kila mara katika kipindi cha mwongo mmoja uliopita, licha ya athari ya kushuka kwa uchumi duniani mnamo 2008. Katika miaka ya hivi majuzi, kiwango cha pesa zilizotumwa zilizopokewa na Kenya kila mwaka kimezidi jumla ya pesa zilizotumwa kutokea ugenini zilizopokewa na nchi zote nyingine za Afrika Mashariki zikiwa zimejumlishwa (KNOMAD, 2019).

Mchoro wa 12. Pesa zilizotumwa Kenya kutoka Marekani, 2010-2017

0 100 200 300 400 500 600 $ milioni 700 17 15 2010

Maelezo: Grafu hii inaonyesha fedha ambazo Wakenya wanaoishi Marekani walituma kutoka ng’ambo kati ya mwaka wa 2010 na 2017 kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya mamilioni ya Dola ya 2019.

Asili: The World Bank’s Bilateral Remittance Estimates.