Sura ya Tatu Je, ni jinsi gani kampuni, mashirika, na watu wa Marekani wanachangia katika ustawi wa Kenya?

Kuna njia nyingi tofauti tofauti ambazo Marekani inatumia kushirikiana na Kenya. Kwenye sura iliyotangulia, tuliangazia misaada ya serikali ya Marekani. Kwenye sura hii, tunaangazia michango ya Marekani kutoka kwenye jamii yake kwa ujumla—kuanzia kampuni ambazo zinahamasisha utoaji wa mtaji kwa ajili ya sekta ya kibinafsi na watekelezaji wa mpango wa kuchangisha fedha kutoka kwa mifuko ya misaada ya kibinafsi, hadi mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofadhili maendeleo ya jamii mashinani pamoja na watu binafsi kupata mapato ambayo yanaimarisha maisha yao.

Tukijumlisha zote, tunakadiria kwamba usaidizi kutoka kwenye kampuni, mashirika na watu binafsi wa Marekani, huchangia takriban Dola bilioni 1.36 kila mwaka kwa uchumi wa Kenya. Michango hii ya kila mwaka inajumuisha takriban: Dola milioni 87.3 kutoka kwenye mifuko ya uhisani wa kibinafsi, Dola milioni 4.6 kwa ajili ya mikopo midogo midogo na michango ya watu binafsi, Dola milioni 270 kwa ajili ya shughuli za NGO, Dola milioni 294.2 kwa ajili ya uwekezaji wa kigeni wa moja kwa moja wa, Dola milioni 190.7 zilizotokana na utalii, na Dola milioni 517.6 zilizotumwa kutoka ng’ambo na Wakenya wanaofanya kazi nchini Marekani. Kwenye sehemu iliyobaki ya sura hii, tunazungumzia kila mmoja ya njia hizi ili kuelewa ni jinsi gani zinawasaidia Wakenya.

Sehemu ya 3.1 Uhisani wa kibinafsi kutoka Marekani na msaada kutoka kwa watu kuelekea kwa watu uliotolewa kwa nchi ya Kenya

Mifuko ya uhisani wa kibinafsi ya Marekani na watu binafsi ni washirika wanaozidi kuwa muhimu sana katika kufanikisha jitihada za Kenya za kuleta maendeleo na ujasiriamali. Mashirika ya hisani huhamasisha fedha kwenye sekta ya kibinafsi ili kufadhili miradi ya maendeleo ya mashinani, pamoja na kutoa msaada muhimu sana kwa mashirika ya kimataifa na asasi za kiraia zinazoendesha shughuli zao nchini Kenya. Kwa upande mwingine, kuimarika kwa teknolojia za habari na mawasiliano kumezidisha mawasiliano na ushirikiano kati ya Wamarekani na wenzao walioko nchini Kenya. Katika sehemu hii, tunaangazia jinsi ambavyo mashirika ya hisani ya kibinafsi ya Marekani na usaidizi unaotoka kwa mtu mmoja hadi mwingine yanasaidia Kenya kutimiza malengo yake ya ustawi na maendeleo yanayoambatana na Ruwaza ya 2030.

Kilichogunduliwa 7: Mifuko saba mikubwa zaidi ya uhisani wa kibinafsi ya Marekani ilifadhili shughuli za maendeleo zenye thamani ya takriban Dola milioni 87.3 kila mwaka, huku ikitilia mkazo sekta za afya, uhakika wa chakula, na utawala bora.

Wahisani wa Marekani ni pamoja na wafadhili saba wa kibinafsi wakubwa zaidi ulimwenguni yaani: Mfuko wa Uhisani wa Arcus (the Arcus Foundation), Mfuko wa Uhisani wa Bill & Melinda (the Bill & Melinda Gates Foundation), Mfuko wa Uhisani wa Conrad N. Hilton (the Conrad N. Hilton Foundation), Mfuko wa Uhisani wa David & Lucile Packard (the David & Lucile Packard Foundation), Mfuko wa Uhisani wa Ford (the Ford Foundation), Mfuko wa Uhisani wa John D. & Catherine T. MacArthur (John D. & Catherine T. MacArthur Foundation), na Mfuko wa Uhisani wa William & Flora Hewlett (the William & Flora Hewlett Foundation). Kwa pamoja, mifuko hii saba ya uhisani ya Kimarekani ilitoa takriban Dola milioni 87.3[22]kwa mwaka kuanzia 2014 hadi 2018 ili kufadhili shughuli za maendeleo nchini Kenya.[23] Hii inajumuisha Dola milioni 76.2 zilizopeanwa moja kwa moja ili kufadhili mashirika ya ndani ya nchi na ya kimataifa yanayoendesha shughuli zao nchini Kenya, pamoja na takriban Dola milioni 11.1 zilizotolewa na Mfuko wa Uhisani wa Bill & Melinda Gates (the Bill & Melinda Gates Foundation) kupitia ufadhili wake kwa Ushirika wa Kimataifa wa Chanjo (Global Alliance for Vaccines, GAVI), Hazina ya Dunia (Global Fund), na Shirika la Afya Duniani (World Health Organization, WHO).

Katika mwaka wa 2018, asilimia 57 ya ufadhili wote kutoka kwa wahisani hawa saba wa Marekani ulielekezwa katika kukuza afya bora na halibora ya raia wa Kenya, kuimarisha shughuli za kilimo, na kuboresha uhakika wa chakula kwa ujumla. Asilimia 11 ya fedha hizi za msaada zilielekezwa katika miradi inayoendeleza jitihada za Kenya za kuimarisha utawala wake na haki za kibinadamu.

Kilichogunduliwa 8: Raia binafsi wa Marekani walihamasisha takriban Dola milioni 4.6 kila mwaka kupitia michango ya kibinafsi na mikopo yenye riba ya chini au isiyokuwa na riba kwa ajili ya kusaidia miradi ya maendeleo nchini Kenya. Fedha hizo zilihamasishwa kwa kutumia majukwa matatu ya kuchangisha fedha mtandaoni kupitia vikundi vikubwa vya watu.

Katika kipindi cha mwongo mmoja uliopita, majukwaa ya kuchangisha pesa kutoka kwa vikundi vikubwa vya watu mitandaoni yameongezeka sana. Majukwaa hayo yanawezesha msaada kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kwa njia mbili—michango na mikopo midogo.

GlobalGiving—ni jukwaa la kuchangishia pesa kutoka kwa vikundi vikubwa vya watu mitandaoni ambalo hukagua na kuwezesha michango kwa ajili ya mashirika ya kijamii ya ndani ya nchi —jukwaa hili linaripoti kwamba asilimia 77 ya zaidi ya Dola milioni 5.6 zilizochangishwa kwa ajili ya miradi ya Kenya na watu binafsi kati ya 2004 na 2019 zilitoka kwa wafadhili wa kutoka marekani. Katika miaka mitano iliyopita, Wakenya walipokea jumla ya michango ya Dola 383,000 kwa mwaka kwa wastani kutoka kwa Wamarekani kupitia GlobalGiving.[24] Michango hii ilifadhili mamia ya miradi katika sekta mbalimbali zikiwemo sekta ya elimu, maendeleo ya kiuchumi na biashara na afya (tazama Mchoro wa 9).

Mchoro wa 9. Jumla ya michango yote kwa Kenya kutoka kwa watoaji misaada binafsi wa Kimarekani kulingana na kategoria ya mradi kwenye jukwaa la GlobalGiving, 2004-2019

Nyinginezo Maendeleo ya kiuchumi na biashara Afya ya kimataifa Elimu Watoto Usawa wa kijinsia & kuwawezesha wanawake $ milioni 1.4 1.4 1.3 0.6 0.3 0.7

Maelezo: “Watoto” ni sekta inayohusiana na sekta hizo nyingine kama ilivyofafanuliwa na GlobalGiving. Miradi iliyopo kwenye kategoria ya “watoto” inaambatana na sekta za Usawa wa kijinsia & kuwawezesha wanawake, elimu na afya. Kiwango cha juu cha misaada kwenye miradi iliyoko katika sekta hii kinaonyesha motisha ya wafadhili katika ufadhili wa watu kibinafsi.Viwango vya pesa vilivyoonyeshwa ni kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya dola ya 2019.

Asili: GlobalGiving.

Majukwaa yanayopeana mikopo midogo kama vile Kiva na Zidisha, yanayounganisha wakopeshaji na wakopaji binafsi wanaohitaji mtaji, yameanza kutumiwa na watu wengi zaidi katika miaka ya hivi majuzi. Wakopaji mara nyingi huwa wanaishi katika maeneo ya mashambani ambapo hapana miundombinu mizuri ya kifedha au ni watu ambao hawawezi kupata mikopo ya kawaida kutokana na vikwazo vingi vilivyopo vya kuomba mikopo. Majukwaa haya yanayopeana mikopo midogo dogo husaidia sana biashara nyingi ndogo ndogo za Kenya na wajasiriamali binafsi kupata mtaji kupitia mikopo yenye riba ya chini.

Kiva ni mojawapo ya majukwaa makubwa kabisa yanayopeana mikopo midogo midogo, huku ikiwa na wakopaji zaidi ya milioni 3.6 katika nchi 76, ikiwemo Kenya. Kwa upande wa Kiva, wakopeshaji binafsi ambao wametambuliwa kuwa wa Kimarekani walitaja kwamba Dola milioni 3.6 zilipeanwa kama mikopo midogo kwa Kenya kwa mwaka kuanzia 2014 hadi 2018. Kiwango hiki, hata hivyo, ni kiwango kidogo kwani jumla ya michango kutoka kwa watumiaji Wamarekani ni nyingi zaidi, kwa vile karibu nusu ya watumiaji wa Kiva huwa hawataji nchi yao asilia wanapofungua akaunti zao. Mikopo mingi zaidi ya Kiva ambayo Kenya ilipokea ilifadhili biashara za kilimo na vyama vya ushirika vya kilimo vya ndani ya nchi kama vile kikundi cha Ann, chama cha ushirika cha wakulima tisa wadogo.

Zidisha ni mfano wa jukwaa dogo zaidi, linalopeana mikopo midogo midogo linaloendesha shughuli zake katika nchi tano tu: Kenya, Ghana, Indonesia, Nigeria, na Zambia. Watumiaji Wamarekani wametoa mikopo ya kiwango wastani cha Dola 611,000 kwa mwaka [25] katika mikopo isiyo na riba kwa wajasiriamali Wakenya kupitia jukwaa la Zidisha.

Kati ya majukwaa haya mawili, Kiva na Zidisha, watumiaji Wamarekani walitoa moja kwa moja mikopo ya kiwango wastani cha Dola milioni 4.2 kwa mwaka kwa Wakenya, [26] katika mikopo yenye riba ya chini au isiyo na riba ili kuwasaidia watu waanzishe na waendeleze biashara ndogo ndogo katika nchi ya Kenya.

Sehemu ya 3.2 Mashirikia ya Marekani yasiyo ya kiserikali yanayoendesha shughuli zao nchini Kenya

The United States is home to approximately 1.5 million non-governmental organizations (NGOs), many of which are actively engaged in supporting overseas development activities. U.S.-based NGOs add value for the Kenyan people in a variety of ways—from direct service delivery and education to advocacy and research. In this section, we examine how U.S. non-governmental organizations active in Kenya are improving livelihoods in line with Kenya’s Vision 2030.

Kilichogunduliwa 9: Zaidi ya Mashirika 1,000 yasiyo ya kiserikali ya Marekani yanayoendesha shughuli zao nchini yalitoa takriban Dola milioni 270 kwa mwaka kwa uchumi wa Kenya, bila kujumuisha misaada kati ya nchi mbili.

Beyond direct giving and microfinance, over 1,000 U.S.-based non-governmental organizations (as of 2017) were actively implementing community-based development projects in Kenya. These non-profit organizations range in scale from small community-based organizations with budgets in the thousands of dollars to organizations with multinational operations and budgets in the hundreds of millions, such as the International Rescue Committee (IRC).

Using tax-filing information for the 2017 tax year from a database of registered U.S. nonprofits, we estimate that over 1,000 U.S.-based NGOs contributed nearly USD 270 million in 2017 to the Kenyan economy through their activities. This amount excludes USD 42 million of U.S. government grants given to these NGOs to implement development projects, as these are already counted in the bilateral aid flows. [27]