Sura ya Pili Je, ni jinsi gani serikali ya Marekani inachangia katika ustawi wa Kenya?

Kenya ni mshirika wa kimkakati na rafiki wa Marekani katika kukuza amani na usalama kote katika kanda ya Afrika Mashariki. Mnamo 2020, nchi hizo mbili zilisherehekea miaka 57 ya mahusiano ya kidiplomasia ambayo yanawezesha ushirikiano wa kiuchumi na wa kimaendeleo, pamoja na ushirikiano katika masuala ya usalama. Serikali ya Marekani inasaidia katika ukuaji na ustawi wa Kenya kwa njia tatu muhimu: (1) msaada kati ya nchi mbili, (2) msaada wa kimataifa, na (3) ukuzaji wa mazingira mazuri ya kubuni sera za kuwezesha biashara, uhamiaji, na uwekezaji.

Kwa jumla, tunakadiria kwamba msaada unaoendeshwa na serikali ya Marekani huchangia takriban Dola bilioni 1.68 kila mwaka katika uchumi wa Kenya. Hiyo inajumuisha Dola bilioni 1 katika msaada wa moja kwa moja kati ya nchi mbili na msaada wa kimataifa kwa mwaka kwa wastani, na pia Dola milioni 678 katika michango isiyo ya moja kwa moja kutoka kwa sera saidizi. Katika sehemu iliyosalia ya sura hii, tunachunguza kila moja ya njia hizi tatu ili kuelewa jinsi zinavyofaidi raia wa Kenya.

Sehemu ya 2.1 Michango ya moja kwa moja ya serikali ya Marekani kuelekea Kenya

Msaada rasmi wa maendeleo (Official Development Assistance, ODA) — pamoja na misaada ya kifedha, mikopo yenye masharti mazuri, na ushauri wa kiufundi — ni njia muhimu zinazotumiwa na serikali ya Marekani kusaidia katika ukuaji na ustawi wa Kenya. Marekani kihistoria imekuwa mshirika mkubwa zaidi wa Kenya katika maendeleo kwa msingi wa kuzingatia mtiririko wa jumla wa msaada kutoka kwa shirika la ODA (OECD-DAC, n.d.). Isitoshe, serikali ya Marekani imekuwa ikiongoza katika kutoa msaada kwa mashirika ya kimataifa (k.m. mashirika ya Umoja wa Mataifa, benki za maendeleo) na kwa hazina za wafadhili wengi zinazofanya kazi nchini Kenya. Katika sehemu hii, tunachunguza jinsi msaada kati ya nchi mbili na msaada wa kimataifa wa Marekani inavyoshirikiana kusaidia raia wa Kenya kuafikia malengo yao yaliyoanishwa katika Ruwaza ya 2030.

Kilichogunduliwa 1: Serikali ya Marekani ilichangia takriban Dola milioni 931 kwa wastani katika msaada kati ya nchi mbili kila mwaka kwa Kenya kwa miaka mitano iliyopita, hasa katika sekta ya afya.

Mawakala na idara ishirini za serikali ya Marekani zimechangia moja kwa moja katika ukuaji na maendeleo ya Kenya tangu 2001.[4] Kati ya hayo, Wakala wa Marekani wa Maendeleo ya Kimataifa (USAID) unaongoza juhudi za Marekani za kati ya nchi mbili katika nyanja muhimu kama vile: kilimo na uhakika wa chakula, elimu, afya, kufanikisha serikali ya ugatuzi kwa faida ya wote, ukuzaji wa amani, mazingira, na ukuaji endelevu wa uchumi (USAID Kenya, n.d).

Kati ya 2001 na 2018, serikali ya Marekani iliongeza msaada wake wa kila mwaka kati ya nchi mbili kwa Kenya mara kumi, kutoka Dola milioni 106 hadi Dola milioni 986.54 (tazama Mchoro wa 1).[5] Katika miaka mitano iliyopita,[6] Marekani imechangia kwa wastani Dola milioni 931 kwa mwaka katika msaada kati ya nchi mbili.

Mchoro wa 1. Msaada kati ya nchi mbili kutoka kwa serikali ya Marekani kwenda Kenya, 2001-2018
200 400 600 800 1,000 $ milioni 1,200 18 15 10 05 2001

Notes: This graph visualizes total U.S. government bilateral assistance disbursements to Kenya each year from 2001 to 2018 in constant USD 2019. These figures include both development assistance and security aid directly given via U.S. government agencies. They exclude assistance given by the U.S. via multilateral agencies that may also benefit Kenya.

Source: USAID Foreign Aid Explorer Data (2001-2018).

Asilimia sitini na mbili ya msaada kati ya nchi mbili kutoka Marekani kwenda Kenya kati ya mwaka wa 2010 na 2018 ililenga sekta ya afya (tazama Mchoro wa 2). Msaada huo unasaidia katika kuimarisha juhudi za serikali ya Kenya katika kutoa huduma za afya za bei nafuu kwa wote. Kwa mfano, mnamo 2017, jumla ya msaada kati ya nchi mbili kutoka serikali ya Marekani ulioenda katika sekta ya afya ulikuwa Dola milioni 598.7. Msaada huo uliongezwa katika kiasi cha Dola milioni 367.5 ambazo Kenya ilihamasisha kutoka vyanzo vya ndani ya nchi ili kukidhi mahitaji yake katika sekta ya afya (Hazina ya Kitaifa, 2017).

Mchoro wa 2. Msaada kati ya nchi mbili uliotolewa kwa Kenya na serikali ya Marekani katika sekta mbalimbali, 2010-2018
Nyinginezo, 2.6% Elimu, 1.7% Demokrasia, haki za binadamu, na utawala, 2.3% Kilimo na uhakika wa chakula , 6.1% Mizozo na vita, 8.7% Maendeleo ya kijamii, 17% Afya, 61.6%

Maelezo: Grafu hii inaonyesha kwa mtazamo wa sekta jumla ya msaada kati ya nchi mbili uliotolewa na serikali ya Marekani kwa Kenya kutoka 2010 hadi 2018 kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya Dola ya 2019.

Asili: USAID Foreign Aid Explorer Data (2010-2018).

Serikali ya Marekani hutoa sehemu kubwa ya msaada wake katika sekta ya afya kuisaidia Kenya kupambana na janga la HIV/UKIMWI. Serikali ya Marekani ndio mfadhili mkubwa zaidi wa mipango ya kuzuia HIV na UKIMWI nchini Kenya (tazama Kikasha cha 1). Isitoshe, Marekani pia imeongeza ufadhili wake tangu 2008 (tazama Mchoro wa 3) kusaidia Kenya kushughulikia masuala mengine ya afya ya kipaumbele, kama vile: kifua kikuu, ugonjwa wa malaria, upangaji uzazi na afya ya uzazi, afya ya mama na watoto, na vitisho vinavyoibuka vya magonjwa ya kuambukiza.

Mchoro wa 3. Msaada kati ya nchi mbili uliotolewa kwa Kenya na serikali ya Marekani katika sekta ya afya, 2001-2018
0 100 200 300 400 500 $ milioni 600 Masuala mengine ya afya HIV/UKIMWI 18 15 10 05 2001

Maelezo: Grafu hii inaonyesha jumla ya msaada kati ya nchi mbili uliotolewa na serikali ya Marekani kwa Kenya kila mwaka kutoka 2001 hadi 2018 kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya Dola ya 2019. Takwimu hizi zinajumuisha misaada ya maendeleo na misaada ya usalama iliyotolewa moja kwa moja kupitia mawakala wa serikali ya Marekani. Hazijumuishi msaada ambao huenda ulifaidi Kenya uliotolewana Marekani kupitia mawakala wa kimataifa.

Asili: USAID Foreign Aid Explorer Data (2001-2018).

Mbali na kuunga mkono vipaumbele vya maendeleo vya muda mrefu vya Kenya kulingana na Ruwaza ya 2030, serikali ya Marekani ilihamasisha msaada wa dharura kusaidia watu wa Kenya kupona kutokana na mshtuko, kama vile kuelekeza Dola milioni 95.6 katika msaada wa chakula kwa Wakenya zaidi ya milioni 4.4 walioathiriwa na Ukame wa Afrika Mashariki wa 2011- 2012 (tazama Kikasha cha 2). Katika Kikasha cha 3, pia tunachunguza kwa makini Dola takriban milioni 85.8 za msaada kati ya nchi mbili kutoka Marekani ambao ulilenga kuwekeza katika idadi inayoongezeka ya vijana wa Kenya kati ya 2009 na 2018.

Kikasha cha 1. Kupambana na HIV/UKIMWI nchini Kenya kupitia utafiti na mipango ya jumla

Ufadhili wa HIV/UKIMWI umekuwa sehemu muhimu ya msaada kati ya nchi mbili kwenda Kenya kufuatia uzinduzi wa Mpango wa Dharura wa Rais wa Msaada wa Ukimwi (PEPFAR) mnamo mwaka wa 2003. Hata hivyo, leo, mwitikio wa Marekani umebadilika ili kujumuisha mipango kadhaa, kama vile mpango wa Msaada Jumuishi wa UKIMWI, Idadi ya Watu, na Afya (APHIAplus) ambayo inachukua mtazamo wa jumla katika masuala ya afya kwa kuchanganya upangaji uzazi, afya ya mama/mtoto, lishe na kuzuia malaria na kifua kikuu ili kujenga mpango mpana zaidi wa huduma za afya kwa kushirikiana na maafisa wa afya wa Kenya. Ikitoa msaada wa kifedha wa zaidi ya Dola milioni 400 kila mwaka, Marekani imesalia kuwa mfadhili mkubwa zaidi wa mpango wa HIV/ UKIMWI nchini Kenya, imezidi wafadhili wengine wote wakiwekwa pamoja.

Ufadhili wa HIV/UKIMWI nchini Kenya kwa mtazamo wa wafadhili, 2009-201
Nyinginezo, 5.6% Hazina ya Dunia (Global Fund), 10% Marekani, 84.4%

Maelezo: Chati hii inaonyesha wafadhili wakubwa zaidi wa Kenya wa kutoa msaada kati ya nchi mbili na msaada wa kimataifa katika kuzuia HIV/UKIMWI na kugharamia matibabu kati ya 2009-2018 kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya Dola ya mwaka wa 2019.

Asili: OECD CRS Database (2009-2018).

Mbali na kufadhili mipango ya afya ya umma nchini Kenya, Idara ya Ulinzi ya serikali ya Marekani pia inasaidia katika utekelezaji wa utafiti muhimu juu ya magonjwa ya kuambukiza nchini Kenya. Taasisi ya Utafiti wa Kimatibabu ya Kenya (KEMRI) imekuwa mwenyeji wa Kitengo cha Utafiti wa Kimatibabu cha Jeshi la Marekani (USAMRD) tangu 1969. Kwa karibu miongo mitano ya kuendesha shughuli zake, maabara hiyo ya utafiti iliyoko jijini Nairobi, na pia vituo vyake vya nyanjani vya Kisumu, Kisian, Kombewa na Kericho, imekuwa mstari wa mbele katika utafiti wa kibaiolojia na kimatibabu ambao umechangia katika utengenezaji wa chanjo muhimu na dawa za kutibu magonjwa kama vile malaria, malale, leishmaniasis, HIV/UKIMWI, na virusi vinavyosambazwa na wadudu kama mbu na kupe.

Kikasha cha 2. Kutoka hali za dharura za njaa hadi kufikia uhakika wa chakula.

Kati ya mwaka wa 2008 na 2018, serikali ya Marekani ilitoa takriban wastani wa Dola bilioni 1.2 (wastani wa Dola milioni 109 kwa mwaka) katika kusaidia kupambana na njaa nchini Kenya chini ya Kifungu cha II cha Sheria ya Marekani ya Chakula kwa ajili ya Amani. Hapo awali, msaada huu ulitilia mkazo utoaji wa moja kwa moja wa chakula kinachozalishwa na Marekani kwa wale walio kwenye hatari ya njaa au kufa njaa. Ingawa misaada mingi ya chakula kutoka Marekani ilitolewa wakati wa Ukame wa Afrika Mashariki wa 2011-2012, Marekani bado ilitoa wastani wa Dola milioni 70.5 kwa mwaka kwa Kenya katika msaada wa chakula chini ya Kifungu cha II kati ya mwaka wa 2014 na 2018. Kadiri ukali wa hali ya dharura ya njaa iliyosababishwa na ukame wa 2011-2012 ilivyopungua, msaada wa Marekani umebadili mwelekeo kutoka kutoa msaada wa chakula cha dharura hadi kuzingatia uhakika wa chakula wa muda mrefu. Mwelekeo huu wa kuzingatia uhakika wa chakula wa muda mrefu unalenga kusaidia jamii kupunguza hatari ya dharura za baadaye kupitia juhudi za kuzuia utapiamlo na kusaidia uzalishaji wa kilimo.

Utoaji wa kila mwaka wa msaada wa chakula wa Marekani chini ya kifungu cha II na msaada wa kilimo kutoka Marekani kwenda Kenya, 2008-2018
0 50 100 150 $ milioni 200 Kilimo na uhakika wa chakula Msaada wa chakula chini ya Kifungu cha II 18 15 10 2008

Maelezo: Grafu hii inaonyesha thamani ya jumla ya kila mwaka ya msaada wa chakula chini ya Kifungu cha II kutoka Marekani kwenda Kenya na thamani ya jumla ya kila mwaka ya msaada wa kilimo kutoka Marekani kwenda Kenya kati ya 2008 na 2018, kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya Dola ya mwaka wa 2019.

Asili: USAID - Food for Peace Funding Overview Fact Sheet (2008-2018) and USAID Foreign Aid Explorer Data (2001-2018).

Kikasha cha 3. Elimu kwa vijana, uongozi, na kujikimu kimaisha

Ikiwa na asilimia 75 ya idadi ya watu walio chini ya umri wa miaka 35 (Baraza, 2020), kuwekeza katika idadi inayozidi kuongezeka ya vijana wa Kenya ni muhimu katika kutimiza azma ya Kenya ya kufikia hadhi ya kuwa taifa la kipato cha kati ifikapo 2030. Kwa ajili ya hiyo, serikali ya Marekani ilihamasisha wastani wa Dola milioni 85.8 katika msaada wa moja kwa moja kati ya nchi mbili kutumika katika mipango inayofaidi vijana wa Kenya kati ya mwaka wa 2009 na 2018. Uwezeshaji wa kiuchumi unaolenga vijana ndio sehemu kubwa zaidi ya msaada huu (asilimia 37), ikifuatiwa na mipango inayotoa makao na mafunzo ya kujikidhi kimaisha, miongoni mwa aina nyingine za msaada, msaada kwa wakimbizi vijana (asilimia 18), na msaada wa kupokea elimu ya msingi na ya juu (asilimia 14).

Msaada wa serikali ya Marekani katika mipango mingi inayolenga vijana unatilia mkazo umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta ya umma na ya kibinafsi kuwekeza katika kizazi kijacho cha viongozi na wafanyakazi. Mpango wa Ajira na Ujuzi kwa Vijana wa Kenya (The Kenya Youth Employment and Skills, K-YES) inatoa fursa kwa viongozi wa sekta ya umma na ya kibinafsi kufanya kazi kwa pamoja kutatua changamoto za ukosefu wa ajira kwa vijana kupitia mipango mahususi ya mafunzo ya kazi ambayo inasaidia vijana kujaza mapungufu ya ujuzi katika tasnia zinazolengwa. Mpango wa The Young African Leaders Intiative (YALI), inashirikiana na vyuo vikuu 40 vya Marekani kufunza ujuzi na kutoa msaada kwa vijana wa Kenya kupitia mradi wake wa Mandela Washington Fellowship Program na The Regional Leadership Centre for East Africa (Kituo cha Uongozi cha Kanda ya Afrika Mashariki) kilichopo Nairobi.

Maelezo: Jumla ya msaada wa moja kwa moja kati ya nchi mbili kutoka Marekani kwenda katika miradi inayoelekezwa kwa vijana ilikadiriwa kwa kutumia kichujio kubaini shughuli ambazo zinataja vijana wazi kwenye jina la mradi. Hili linaweza kuwa kadirio la chini lisilo sahihi la thamani ya jumla ya Dola za Marekani zilizofaidi vijana wa Kenya. Takwimu zote za fedha zilizotolewa zimewekwa kwa msingi wa thamani isiyobadilika ya Dola ya 2019. Asili: Foreign Aid Explorer (2009-2018).